
Dar es Salaam. Watu wenye ulemavu wa ngozi (albino), jana walizua tafrani Kituo cha Polisi Buguruni, wakipinga dhamana kwa mshtakiwa, Ombeni Swai (34), mkazi wa Tabata Matumbi anayekabiliwa na kesi ya kutoa vitisho vya kumuua mwenzao. Tafrani hiyo ilianzia katika Mahakama ya Mwanzo Buguruni baada ya mshtakiwa huyo kusomewa mashtaka na Karani wa Mahakama, Edwin Wandanda na kisha...

Moshi. Kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Francis amekubali kumuondolea sakramenti ya upadri, Raymond Mosha wa Jimbo Katoliki la Moshi ikiwa ni miaka 20 tangu padri huyo aombe kuachana na daraja hilo. Barua ya uamuzi wa Papa Francis ilisomwa juzi katika parokia na vigango vyote vya Kanisa Katoliki Jimbo la Moshi katika ibada zilizofanyika katika makanisa ya jimbo...

Dar es Salaam. Aliyekuwa Mwenyekiti wa kwanza wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), tangu kuanzishwa kwake mwaka 1993 chini ya mfumo wa vyama vingi, Jaji Lewis Makame amefariki dunia. Taarifa iliyopatikana jana jioni na kuthibitishwa na mwanaye, Eugene Makame, Jaji Makame alifariki dunia jana mchana katika Hospitali ya AMI Trauma, Masaki Dar es Salaam alikokuwa amelazwa kwa...

Dunia imeukaribisha mwaka mpya wa 2014 kwa fataki, chereko, shangwe kubwa na kutakiana kheri. Sherehe kubwa zilizofanyika Dubai na mji mkuu wa Ujerumani, Berlin ni mfano wa zile zilizotia fora Dubai imevunja rekodi ya dunia kwa maonyesho makubwa kabisa ya fataki kuwahi kushuhudiwa katika Mkesha wa Mwaka Mpya yaliyohusisha fashifashi nusu milioni. Fataki hizo zilin'gara angani kwa...

Hali ya kiafya ya waziri mkuu wa zamani wa Israel, Ariel Sharon - ambaye amekuwa katika hali mahututi, inaendelea kuzorota zaidi. Inaarifiwa kwamba maisha yake yamo hatarini. Madaktari wanasema kuwa Sharon mwenye umri wa miaka , 85, anakabiliwa na matatizo ya afya ya viongo vyake vya mwili ikiwemo Figo zake na kwamba vinaanza kuonekana kutofanya kazi vyema. Hata...

Mapigano yanaendelea nchini Sudan Kusini licha ya pande mbili zinazohusishwa na mgogoro wa nchi hiyo kujiandaa kwa mazungumzo ya amani nchini Ethiopia. Msemaji wa jeshi la Sudan Kusini ameiambia BBC kuwa mapigano yanaendelea katika mji wa Bor na baadhi ya sehemu za jimbo la Unity. Pande zote mbili za serikali na waasi wamepeleka wajumbe wao katika mji mkuu...

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimwapisha Inspekta Generali wa Polisi (IGP) mpya Afande Ernest Mangu katika viwanja vya Ikulu jijini Dar es salaam. Singida. Mama Mzazi wa Mkuu wa Polisi nchini (IGP), Ernest Mangu, Mwanaidi Msengi, amemsihi mwanawe kufanya kazi kwa bidii asimwangushe Rais Jakaya Kikwete ili asije kujutia kumpa nafasi hiyo. Mwanaidi alisema licha ya furaha kubwa aliyonayo, ...

Wadhifa wa Urais wa Tanzania umeendelea kujikuta njia panda kila unapofika wakati wa kuidhinisha kutekelezwa kwa adhabu ya kifo kwa waliohukumiwa kunyongwa hadi kufa na mahakama, na suala hilo limekuwa gumu kutekelezwa katika awamu zote nne za uongozi. Hukumu hiyo ni kama haitekelezeki na pengine mafaili yaliyobeba uamuzi wa mahakama wenye adhabu za vifo, yameendelea kusubiri kusainiwa tangu...

Kundi la kieneo barani Afrika linasema serikali ya Sudan Kusini imekubali kusitisha mapigano hatua ambayo itasaidia kumalizika kwa mapigano ya makabila mbali mbali ambayo yamesababisha vifo vya zaidi ya watu 1,000 mwezi huu. Jumuiya ya nchi za pembe za Afrika- IGAD ilitangaza uamuzi huo mwishoni mwa mkutano uliofanyika ijumaa mjini Nairobi. Kundi hilo liliwasihi wafuasi wa Makamu Rais...

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amewasili nchini jana, Ijumaa, Desemba 27, 2013, akitokea New York, Marekani. Rais Kikwete amekuwa New York kwa wiki moja kwa shughuli za kufanyiwa uchunguzi wa afya yake. Kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere mjini Dar es Salaam, Rais Kikwete amelakiwa na viongozi mbali mbali...

Takriban wanajeshi watano na afisa wa jeshi wameuawa katika mlipuko wa bomu mjini Mogadishu,nchini Somalia mashuhuda wameeleza. Mlipuko huo unaelezwa kutokea wakati wanajeshi hao wakipata malipo yao nje kidogo ya mji huo. Sababu ya mlipuko huo haijafahamika,majeruhi kadhaa wamepelekwa hospitalini kwa matibabu. Wanamgambo wa kiislamu, al Shabab walitimuliwa kwa nguvu mjini Mogadishu mwaka 2011 lakini wameendelea kufanya mashambulizi...

Papa Francis wa kanisa Katoliki duniani amesherehekea siku yake ya kuzaliwa kwakuwakaribisha watu wasiojiweza wanne ambao walijumuika na wageni wengine pamoja na Papa kupata kifungua kinywa alichoandaa mahususi kwa kutimiza miaka 77 tangu azaliwe, katika makazi ya Mtakatifu Martha yaliyopo Vatican nchini Italia. Papa Francis aliwaalika watu hao pamoja na wafanyakazi wa Vatican waliojumuika na familia zao katika...