Dar es Salaam. Watu wenye ulemavu wa ngozi (albino), jana walizua tafrani Kituo cha Polisi Buguruni, wakipinga dhamana kwa mshtakiwa, Ombeni Swai (34), mkazi wa Tabata Matumbi anayekabiliwa na kesi ya kutoa vitisho vya kumuua mwenzao.
Tafrani hiyo ilianzia katika Mahakama ya Mwanzo
Buguruni baada ya mshtakiwa huyo kusomewa mashtaka na Karani wa
Mahakama, Edwin Wandanda na kisha Hakimu Mfawidhi, Benjamin Mwakasonda
aliyekuwa akiisikiliza kusema dhamana ya mshtakiwa iko wazi.
Ingawa mshtakiwa alishindwa kutimiza masharti ya
dhamana, albino waliokuwapo mahakamani hapo hawakufurahishwa na kitendo
cha kuwapo kwa nafasi ya dhamana kwa mshtakiwa wakidai kwamba ameshatoa
vitisho vya mauaji dhidi yao.
Baada ya kulalamika mahakamani hapo waliandamana
hadi kituoni hapo ambako mshtakiwa alikuwa amepelekwa hali
iliyosababisha polisi kituoni hapo kutumia risasi za baridi kuwatawanya
na kusababisha taharuki kwa wafanyabiashara na wakazi wa eneo hilo.
Mwandishi wetu alishuhudia baadhi ya watu wakiwa wamesimama, wengine wakikimbia ovyo huku polisi wakiwa silaha.
Kamanda wa Mkoa wa Polisi Ilala, Mariam Nzuki alisema vurugu hizo ziliongezeka baada ya kundi la vijana wa sokoni kuungana nao.
Alisema baada ya polisi kuona hivyo, walitumia mabomu ya machozi kuwatawanya na kumpeleka mtuhumiwa katika Mahabusu ya Segerea.
Hati ya mashtaka
Mshtakiwa anadaiwa kuwa Agosti 16, mwaka huu
maeneo ya Buguruni kwa Mkanda alitishia kuua kwa maneno watu wenye
ulemavu wa ngozi katika maeneo hayo.
Hati hiyo inadai kuwa mshtakiwa alimtishia kwa maneno mlalamikaji, Mwinyiusi Issa kuwa atamuua kama anavyoua albino.
Mengi ajitolea
- Kwa wanaolilia uhusiano wa mapenzi na wageni au wazungu-2
- Harakati za kuadhimisha Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia zinatufunza nini? -1
- Je, walimu wetu wameandaliwa kuikomboa jamii?
- Lawama ziende kwa wajumbe wa Katiba, si Rais Jakaya Kikwete
- Mazingira ya kusikitisha ya utoaji wa elimu ya awali Kigoma
- Sure Boy agoma penalti
- Hapatoshi APR, Rayon Sports, Rwanda kusimama dakika 90
- ‘Simba ya Phiri ina kasoro tatu’
- ‘Sheria kali uvuvi haramu zitolewe’
- GST yataka usafirishaji madini ghafi usitishwe
- Lipumba: Moyo wetu Ukawa ni wajumbe 14
- Uamuzi mgumu CCM katika Kamati Kuu leo
- Hoja za Jaji Warioba mateso Bunge Maalumu
- Mbatia asema kauli ya Werema imejaa unafiki
- Papa amruhusu Padri Mosha kuoa
- Gari lililobeba maiti kumi laua wawili Mikese
- Serikali yatangaza nafasi za kazi 1,100
- Katiba Mpya hakieleweki
- Misimamo ya vigogo Katiba Mpya
- Uraia pacha, masilahi binafsi dhidi ya masilahi ya Taifa
- Lipumba: Ujana siyo sifa ya urais
0 comments:
Chapisha Maoni