Jumamosi, 28 Desemba 2013

RAIS JAKAYA KIKWETE AREJEA KUTOKA MAREKANI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amewasili nchini jana, Ijumaa, Desemba 27, 2013, akitokea New York, Marekani.
Rais Kikwete amekuwa New York kwa wiki moja kwa shughuli za kufanyiwa uchunguzi wa afya yake.
Kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere mjini Dar es Salaam, Rais Kikwete amelakiwa na viongozi mbali mbali wakiongozwa na Makamu wa Rais, Mheshimiwa Dkt. Mohammed Gharib Bilal.
 
 
Makamu wa Rais Dk.Mohamed Gharib Bilal akimlaki Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete muda mfupi baada ya Kuwasili nchini akitokea jijini New York Marekani ambapo alikwenda kwa ukaguzi wa kawaida wa afya yake.Akiwa nachini Marekani Rais Kikwete alialikwa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Bwana Ban ki Moon nakufanya naye mazungumzo kuhusu ushiriki wa majeshi ya Tanzania katika ulinzi wa Amani katika nchi mbalimbali.

Makamu wa Rais Dk.Mohamed Gharib Bilal akizungumza na Rais Dkt.Jakaya Kikwete Mrisho mara baada ya kumlaki muda mfupi baada ya Kuwasili nchini akitokea jijini New York Marekani ambapo alikwenda kwa ukaguzi wa kawaida wa afya yake nchini Marekani. Rais Kikwete alialikwa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Bwana Ban Ki Moon na kufanya naye mazungumzo kuhusu ushiriki wa majeshi ya Tanzania katika ulinzi wa Amani katika nchi mbalimbali.

0 comments:

Chapisha Maoni

Call Us Now:

+255 655 732121, +255 716 758595 / +255 762 758595