Papa Francis aliwaalika watu hao pamoja na wafanyakazi wa Vatican waliojumuika na familia zao katika makazi hayo ambayo amekuwa akiishi tangu achaguliwe kuwa Papa ambayo pia yamekuwa yakikaliwa na mitume na viongozi mbalimbali wa kanisa hilo. Kwa mujibu wa ripoti iliyotolewa na radio ya Vatican imeendelea kuripoti kwamba watu hao ni kati ya kundi kubwa la watu wasio na makazi ambao hulala nje ya viunga vya Mtakatifu Peter.
Aidha katika picha zilizotolewa zimemuonyesha Papa Francis akizungumza na watu watatu kati ya wanne aliowaalika akiwemo mmoja aliyeonekana akiwa amembeba mbwa. Taarifa ya Vatican imesema tukio hilo lilikuwa lakirafiki zaidi huku waziri wa mambo ya ndani wa Vatican Pietro Parolin amemtakia heri Papa Francis katika siku yake ya kuzaliwa.
![]() |
Papa akiwa na watu wasio na makazi nje ya Vatican |
0 comments:
Chapisha Maoni