Alhamisi, 2 Januari 2014

JESHI LA POLISI LAPATA IGP MPYA

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimwapisha Inspekta Generali wa Polisi (IGP) mpya Afande Ernest Mangu katika viwanja vya Ikulu jijini Dar es salaam.

Singida. Mama Mzazi wa Mkuu wa  Polisi nchini (IGP), Ernest Mangu, Mwanaidi Msengi, amemsihi mwanawe kufanya kazi kwa bidii asimwangushe Rais Jakaya Kikwete ili asije kujutia kumpa nafasi hiyo.
Mwanaidi alisema licha ya furaha kubwa aliyonayo,  anamuasa mtoto wake kuchapa kazi kwa bidii kama njia mojawapo ya shukurani kwa Rais Kikwete kwa kumteua akiwa mwenyeji  wa kwanza kutoka Mkoa wa Singida kushika wadhifa huo nyeti.
“Hii ni heshima kubwa sana kwangu binafsi, ndugu zake, wakazi wa Kijiji cha Kihunadi na Mkoa wa Singida, kwa hiyo lengo langu ni kumwombea mtoto wangu Mangu asimwangushe Rais... Eee Baba (Mungu) msaidie mwanangu atimize wajibu wake ipasavyo ili Rais Kikwete siku moja aseme hakukosea kumpa Mangu ukuu wa polisi,” alisema Mwanaidi.
Juzi ndugu, jamaa na marafiki walifanya hafla ndogo iliyoambatana na vifijo, nderemo na bashasha na wakazi wa Kijiji cha Kihunadi, Tarafa ya Ilongero, mkoani Singida, alikozaliwa IGP huyo huku wakidai sasa kijiji chao kitajulikana haraka ndani na nje ya Tanzania.
Walisema licha ya kujulikana, changamoto mbalimbali zinazokikabili kijiji hicho zitapatiwa ufumbuzi wa kudumu mapema iwezekanavyo.
Mwanaidi alisema Mangu alianza kumwonyesha mafanikio tangu Shule ya Msingi Kinyagigi, kwani alikuwa na bidii ya kujisomea mara kwa mara alishika nafasi ya kwanza au  ya pili.
Kwa mujibu wa Mwanaidi, IGP Mangu ni mtoto wa pili kati ya saba aliowazaa.
 “Mangu ni wa pili kati ya watoto wangu saba baada ya kuolewa na baba yao, Jumbe Omari Mangu aliyefariki Aprili 27, 1988.  Jina la Jumbe linatokana na kupewa kazi ya ujumbe wa wakoloni wakati wa ujana wake,” alisema.
Wenyeji wa kijiji hicho, walisema  wamekuwa wakiamini Mangu atafika mbali kwa kushika nafasi za juu za uongozi, kutokana na uadilifu, uchapaji kazi, ukaribu wake na wananchi, uaminifu na uwazi.
Mwanaidi alisema Mangu alipofaulu kwenda sekondari alilazimika kuomba ng’ombe kwa mke mweza, ili akamuuze apate fedha za kugharimia masomo ya mtoto wake.
“Mke mwenzangu alimtoa ng’ombe wake, lakini  Mangu alipomuuza kwenye mnada pale Singida mjini, aliibiwa fedha zote na alirudi nyumbani akilia sana,” alisema.
Alisema baada ya hapo alimwambia mtoto wake kwamba, ataanza kutengeneza vyungu kwa kutumia udongo wa mfinyanzi  ili kupata fedha za kugharimia masomo yake. “Nashukuru Mangu alinielewa vizuri kwa sababu alishiriki kubeba kichwani vyungu hivyo wakati wa kuviuza hadi kichwa chake kilikaribia kuwa kipara.  Nilibuni chanzo kingine cha mapato ambacho kilikuwa ni kukoroga na kuuza pombe za kienyeji,” alisema. Inadaiwa baba yake, IGP  Mangu alioa wanawake sita kwa nyakati tofauti, lengo likiwa ni kupata mtoto wa kiume.  Wengi wa wake zake walikuwa wakizaa watoto wa kike

3 comments:

  1. Maoni haya yameondolewa na mwandishi.

    JibuFuta
  2. Maoni haya yameondolewa na mwandishi.

    JibuFuta
  3. Maisha yangu Maajabu yanashangaza ushuhuda, Jinsi nimepata kisanduku chenye nguvu sana ambacho sasa ni pesa yangu mara mbili kutoka mia hadi elfu ya pesa ndani ya masaa 24, na pia jinsi nimerudisha mpenzi wangu wa zamani, sababu kuu niliwasiliana na Dk Lomi kwa msaada mimi kumrudisha mpenzi wangu wa zamani, basi ananisaidia ni nguvu kubwa ya kumrudisha mpenzi wangu wa zamani, na ananipenda na ananithamini sasa, basi mimi na Dr Lomi tukawa marafiki, baada ya mazungumzo kadhaa namuuliza ikiwa kuna njia anaweza kuniganga ili nipate pesa, hapo ndipo aliponiambia juu ya sanduku hili la uchawi, akaniambia kuna aina na saizi tofauti ya sanduku, aliniambia aina zote za sanduku, ningeweza kumudu ndogo tu ya sanduku, baada ya maombi muhimu anayofanya kwenye sanduku, ananipeleka kupitia huduma ya kujifungua, aliniambia niweke pesa ndani, niliweka ndani ya sanduku 100 euro baada ya masaa 24 nikagundua ilikuwa elfu 10 euro ndani, na nimekuwa nikitumia sanduku kwa miezi 7 sasa, mimi na mchumba wangu tunaishi maisha bora, ikiwa unahitaji b ack mpenzi wako au pesa spell wasiliana na Dr Lomi kwa barua pepe: lomiultimatetemple@gmail.com au WhatsApp namba +2349034287285 unaweza pia kumwandikia kupitia Jina la Mtumiaji la Snapchat: drlomi20 atakusaidia nje, asante kwa kusoma

    Kwaheri Gerd Ulrich

    JibuFuta

Call Us Now:

+255 655 732121, +255 716 758595 / +255 762 758595