KUONDOKANA na umasikini uliopo, wadau wa kilimo wametakiwa kutafuta njia
nafuu zitakazosaidia matumizi ya vipimo na viwango sahihi
vitakavyowanufaisha wakulima. Kauli hiyo ilitolewa Dar es Salaam juzi na
Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Joyce Mapunjo, wakati
akifungua warsha ya matumizi sahihi ya vipimo na viwango.
Warsha hiyo iliyoandaliwa na muungano ya Asasi ya Tanzania Markets
Policy Action Nodes (TM-PAN) na kufadhiliwa na Shirika la Alliance for
Green Revolution in Africa (AGRA) ililenga kujadili taarifa za utafiti
wa vipimo uliofanyika nchini hivi karibuni.Alisema masuala ya
vipimo vinashughulikiwa na Wakala wa Vipimo (WMA) na kuna umuhimu wa
kuhakikisha inajumuisha wadau wengi kwa ajili ya kuleta maendeleo.Aliwataka
wadau hao kujadili namna ya kuhakikisha watu wote wanakuwa na uelewa wa
kutosha kuhusu viwango hasa vile vinavyohusiana na chakula.
“Kwa
hiyo ni muhimu kuhakikisha kuwa viwango vinafahamika vizuri kabla
hatujaingia katika gharama kubwa ya matibabu itakayotokana na matumizi
yasiyo sahihi ambayo yanaweza kuepukwa,” alisema Mapunjo. Alitoa
changamoto kwa wadau hao kuhakikisha wanatoa mapendekezo
yanayotekelezeka, wazi na yatakayoweza kuisadia Serikali kufikia malengo
ya muda mrefu.
Akitoa matokeo ya utafiti huo, mtafiti kutoka
Shirika la MRA Associates, Charles Ogutu, alisema utafiti umebaini kuwa
bado hakuna mfumo unaoeleweka unaodhibiti matumizi sahihi ya vipimo na
viwango. Alisema miongozo mingi na kanuni imeandikwa kwa lugha isiyoeleweka kwa mkulima wa kawaida. Alisema
katika utafiti huo, wamebaini kodi za mazao na masoko zinatozwa
kulingana na idadi ya magunia badala ya uzito hivyo inatoa mwanya kwa
wafanyabiashara kujaza lumbesa. Alisema utafiti umeonyesha kuwa
taasisi za kiserikali kama WMA, Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) na
Shirika la Viwango Tanzania (TBS) vina idadi ndogo ya rasilimali watu.
“Kuna
baadhi ya mikoa na wilaya utakuta watumishi wawili, bila nyenzo za
usafiri sasa unatarajia wataweza kufanya kazi inavyotakiwa,” alihoji
Ogutu. Akichangia kuhusu utafiti huo, Mratibu wa TM-PAN, Braison
Sali, aliishauri Serikali kushughulikia changamoto zote zilizoainishwa
na kuongeza bajeti katika kilimo. “Ushauri wangu kwa wakulima ni
kuelimishwa zaidi kuhusiana na ujanja unaofanywa na baadhi ya
wafanyabiashara kupitia lumbesa na kuanzishwa kwa mpango wa kuhifadhi
vyakula katika maghala kwa kuzingatia ubora,” alisema Ogutu.
Jumatatu, 24 Juni 2013
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Call Us Now:
+255 655 732121,
+255 716 758595 / +255 762 758595
0 comments:
Chapisha Maoni