Jumatatu, 1 Julai 2013

OBAMA AKANYAGA ARDHI YA TANZANIA, MAELFU WAMPOKEA

Rais Barack Obama wa Marekani amewasili hapa nchini leo majira ya saa nane na dakika 20 alasiri akitokea nchini Africa kusini, wito wake wakwanza amemtaka Rais Jakaya Kikwete kuendelea na jitihada zake za kusuluhisha migogoro Congo DRC, Rais Obama ametoa kauli wakati akijibu swali la mwandishi wa habari wa Nation wa nchini Congo aliyetaka kujua msimamo wa Marekani kuhusu mgogoro wa congo uliodumu zaidi ya miaka 20
Akijibu swali alisema, aliyepaswa kujibu swali hili ni Rais Kikwete kwakuwa yeye ndiye anayeshughulikia migogoro ya nchi za maziwa makuu. Hata hivyo alimtaka Rais Kikwete kukaa na Rais Kabila na kuangalia ni jinsi gani wanavyoweza kuondokana na hali hiyo nchini Congo na hasa ukizingatia kwamba migogoro Congo DRC inatokana na maslahi, huo ulikuwa mkutano wa kwanza wa Rais Obama na waandishi wa habari wa ndani na nje katika ziara yake hapa nchini Tanzania.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimtambulisha kwa Rais Barrack Obama wa Marekani Rais wa Zanzibar Dr.Ali Mohamed Shein muda mfupi baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam leo mchana.Huku Mke wa Rais Mama Salma Kikwete na Mke wa Rais wa Marekani Michelle Obama Wakiangalia
 
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete na mgeni wake Mama Michelle  Obama muda mfupi baada ya kuwasili kwa Rais Obama nchini kwa ziara ya siku mbili nchini.
  Mapokezi ya Rais Obama na mkewe Michelle yalivyokuwa mara baada ya kuwasili ikulu jijini Dar es salaam, ilikuwa na shangwe na vigelegele
Rais Obama akipanda mti aina ya mpingo katika viwanja vya Ikulu jijini Dar es salaam leo 

0 comments:

Chapisha Maoni

Call Us Now:

+255 655 732121, +255 716 758595 / +255 762 758595